Home Soka Waziri Jr Atimkia Dodoma Jiji

Waziri Jr Atimkia Dodoma Jiji

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji Waziri Junior ameisaini katika klabu ya Dodoma Jiji FC kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea KMC FC ambapo amemaliza mkataba wake msimu huu ulioisha wa ligi kuu.

Awali Pamba Jiji FC ilionesha nia ya kumsajili Waziri Junior na ikamtumia hadi nauli ya kwenda jijini Mwanza kusaini mkataba wa Pamba Jiji FC ila hakwenda na badala yake akasaini Dodoma Jiji FC, baada ya kuvutiwa na ofa yao nono.

Waziri nje na timu hiyo pia amepata ofa nono nchini Qatar ambapo kuna timu ambayo inashiriki ligi daraja la kwanza imevutiwa na uwezo wa mshambuliaji huyo huku kukiwa na urahisi zaidi kuvunja mkataba wake na Dodoma Jiji kutokana na kuwepo na kipengele cha kumruhusu kuondoka iwapo atapata timu nje ya nchi.

banner

Waziri ni moja ya washambuliaji hatari wazawa nchini ambapo ana uwezo mkubwa zaidi wa kufunga mabao makali huku msimu huu ulioisha akiwa na Kmc alifanikiwa kufunga jumla ya mabao 12 katika ligi kuu ya soka ya Nbc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited