Home Makala Wydad Ac Yamsajili Mwalimu

Wydad Ac Yamsajili Mwalimu

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Wydad Athletic Club imefanikiwa kuinasa saini ya mshambuliaji Selemani Mwalimu kutoka klabu ya Singida Black Stars baada ya kufikia makubaliano na timu hiyo kumsajili staa huyo mwenye mabao sita katika ligi kuu ya Nbc nchini.

Kocha Rulani Mokwena alikua na uhitaji mkubwa wa mshambuliaji wa kati ambapo alianza kumnyemelea mshambuliaji wa klabu ya Yanga sc Clement Mzize lakini baada ya dili hilo kushindikana aliamua kumsajili Mwalimu.

banner

Tayari klabu yake ya Singida Black Stars imethibitisha kukamilika kwa dili hilo la mshambuliaji huyo aliyekua anaichezea Fountain Gate Fc kwa mkopo wa mwaka mmoja.

Mwalimu amesajili kwa dau linalokadiriwa kufikia kiasi cha shilingi milioni mia nane kwa mkataba wa miaka minne huku kukiwa na kipengele cha Singida Black Stars kupata asilimia kumi ya mauzo ya baadae.

Kwa upande wa maslahi binafsi pamoja na bonansi mbalimbali staa huyo pia atapokea mshahara wa milioni sita kwa mwezi katika mwaka wake wa kwanza wa mkataba huo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited