Home Soka Yanga Sc Yamfukuzia Silla Kimya Kimya

Yanga Sc Yamfukuzia Silla Kimya Kimya

by Sports Leo
0 comments

Mabosi wa klabu ya Yanga sc wamevutiwa na uwezo wa winga wa Azam Fc Gibril Sillah ambaye mkataba wake uko mbioni kumalizika katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Yanga sc inafanya ushawishi wa kimyakimya kuhakikisha inampata Djibril Sillah, Winga wa Azam mwisho wa msimu huu ikitaka dili hilo limalizike kwa haraka kabla ya ligi kumalizika.

Sillah Mkataba wake unafika ukingoni mwisho wa msimu huu mpaka sasa hajassini mkataba mpya katika klabu hiyo huku mazungumzo baina yake na mabosi wa Azam Fc yakiwa bado hawajafikia muafaka.

banner

Yanga wanahitaji Winga anayetumia mguu wa kushoto na wanaona winga huyo aliyewafunga mara kadhaa kuwa anafaa kuchukua nafasi hiyo.

Kazi kubwa inafanyika kumtengea dau la maana staa huyo ili kumshawishi kutua jangwani japo mabosi wa klabu yake ya sasa wanapambana kumbakisha.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited