Home Makala Yanga Sc Yanukia Robo Fainali Cafcl

Yanga Sc Yanukia Robo Fainali Cafcl

by Sports Leo
0 comments

Ushindi wa 1-0 ulioupata klabu ya Yanga sc dhidi ya Klabu ya Al Hilal Omdurman ya Sudan umeiweka timu hiyo katika matumaini makubwa ya kufuzu robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika katika mchezo uliofanyika nchini Mauritania.

Yanga sc sasa inapaswa kushinda mchezo ujao dhidi ya Mc Algers utakaofanyika nchini katika uwanja wa Benjamin Mkapa siku ya Jumamosi Januari 18 2024.

Bao pekee la mapema la kiungo mshambuliaji Stephan Aziz Ki lilidumu mpaka dakika ya mwisho ya mchezo huo mgumu na wenye kasi kubwa.

banner

Uzembe wa viungo wa Al Hilal kutomkaba Azizi Ki aliyepiga shuti kali lililozama wavuni moja kwa moja dakika ya saba ya mchezo huo.

Kila upande ulikua na uwezekano wa kupata bao kutokana na timu hizo kushambuliana kwa zamu kila mara hali iliyosababisha mchezo huo kutotabirika kirahisi.

Prince Dube alikosa nafasi kadhaa za mabao baada ya kushindwa kumchungulia kipa Fofana aliyekua kikwazo kwa Yanga sc.

Yanga sc sasa imefikisha alama saba ikiwa nyuma ya Al Hilal Fc yenye alama 10 ikiwa imeshafuzu huku Mc Algers ikiwa na alama nane ikiwania kufuzu endapo itapata sare ama kudhi

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited