Kinda wa Barcelona Ansu Fati ameiongoza klabu yake kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Valencia katika mchezo wa ligi kuu soka nchini Hispania(La liga) uliofanyika katika dimba la Camp Nou Jijini Barcelona.
Memphis Depay aliiongezea Barcelona goli la pili kwa mkwanju wa penati dakika ya 41 baada ya Asu Fati kufanyiwa madhambi ndani ya penati box na mlinzi Gaya.
Philipe Coutinho aliyeingia kipindi cha pili aliihakikishia ushindi timu yake kwa kufunga goli la tatu dakika ya 85 na kumaliza ukame wa takribani miezi 11 bila kufunga goli la ligi.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Barcelona wamepanda ya saba kwenye La liga wakiwa na pointi 15 pointi tano nyuma ya vinara Real Sociedad wenye alama 20 huku Barca wakiwa na faida ya mchezo mmoja mkononi.