Klabu ya Azam fc imefungwa bao 1-0 dhidi ya Kmc katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliofanyika katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaam.
Reliants Lusajo alisababisha Azam Fc kupoteza mchezo wa pili wa ligi kuu baada ya kufunga bao pekee dakika ya 57 na kuipa alama tatu Kmc.
Azam Fc licha ya kupoteza mchezo huu badp wanabaki kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa na alama 26 huku Yanga sc wakiwafatia wakiwa na alama 24 na Simba sc wakiwa katika nafasi ya tatu wakiwa na alama 23.