Home Soka Chama,Miqquison Waikosa Azam Fc

Chama,Miqquison Waikosa Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Mastaa Cletous Chama,Luis Miqquison na Saido Ntibanzokiza wataukosa mchezo wa ligi kuu dhidi ya klabu ya Azam Fc utakaochezwa leo Mei 9 katika uwanja wa Benjamin Mkapa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo adhabu na majeraha.

Kikosi cha Simba sc kinachoshuka uwanjani katika mchezo huo kimetangazwa huku mastaa hao sambamba na Henock Inonga Baka wakiwa hawapo ambapo inafahamika kuwa Chama anatumikia adhabu ya kufungiwa na mamlaka za soka michezo mitatu huku Saido na Luis Miqquison wakisumbuliwa na majeraha.

banner

Simba sc inashuka dimbani dhidi ya Azam Fc kutafuta alama tatu muhimu ambazo zitaipa faida ya kumaliza nafasi ya pili ya msimamo wa ligi kuu nchini ambapo endapo itafanikiwa kuifunga Azam Fc katika mchezo huo itapunguza alama tatu zaidi na kuweka mazingira mazuri ya nafasi hiyo maana Yanga sc mpaka sasa ina asilimia tisini kuchukua ubingwa wa ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited