Klabu ya Simba sc inatajwa kumalizana na kiungo wa timu ya Fc Platnum Perfect Chikwende wakiipiku Azam Fc iliyokuwa imekaribia kumnasa taarifa zinaripoti zaidi.
Inadaiwa awali Azam Fc ilitakiwa kutoa kiasi cha shilingi milioni 116 ambazo zilihitajika kuvunja mkataba wa kiungo huyo mshambuliaji lakini mabosi wa Azam Fc walichelewa kukamilisha malipo hayo hivyo Simba sc wakaipiku baada ya kuweka mezani kiasi cha shilingi milioni 127.
Chikwende amekua maarufu nchini tangu alipofunga bao dhidi ya Simba sc katika mchezo wa hatua ya mtoano klabu bingwa barani Afrika uliofanyika nchini Zimbabwe.