Site icon Sports Leo

Dickson Job Atua Yanga sc

Klabu ya Yanga sc imekamilisha usajili wa beki kinda wa Mtibwa sugar Dickson Job akisaini mkataba wa miaka miwili na nusu kukipiga Jangwani.

Mchezaji huyo hatimaye amesaini baada ya tetesi za muda mrefu kutua klabuni hapo kusambaa lakini leo mchana huu klabu ya Yanga sc kupitia kurasa za mitandao ya kijamii zimetoka taarifa rasmi za dili hilo kukamilika.

Job atakutana na kazi ngumu ya kuchukua nafasi kutoka kwa Bakari Mwamnyeto na Lamine Moro huku katika benchi kukiwa na Abdalah Shaibu na Juma Said Makapu.

Exit mobile version