Klabu ya Manchester United imethibitisha kuwa itamkosa beki wake wa kati Mfaransa Rafael Varane kwa wiki kadhaa kutokana na maumivu kwenye eneo la kinena wkati akiitumikia timu yake ya Taifa ya Ufaransa kwenye mchezo wa fainali wa michuano ya ligi ya Mataifa Ulaya.
Katika mchezo huo Varane aliumia kipindi cha pili na kushindwa kuendelea ambapo nafasi yake ilichukuliwa na beki wa Bayern Munich Dayot Upamecano.
Beki huyo amekuwa mhimili muhimu katika kikosi cha Man Utd tangu kusajiliwa katika dirisha lililopita akitokea Real Madrid na ametengeneza kombinesheni nzuri kati yake na nahodha wa timu hiyo Harry Maguire.
Hili ni pengo kubwa sana kwa Mashetani Wekundu kwani tayari inamkosa nahodha wake Harry Maguire kwa maumivu ya kigimbi cha mguu,hivyo kuwa na wakati mgumu kuelekea ratiba ngumu ya mwezi huu wa Oktoba.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Timu hiyo sasa itawategemea zaidi mabeki Eric Bailly na Victor Lindelof katika safu ya ulinzi pamoja na majeruhi wa muda mrefu Phil Jones aliyerejea hivi karibuni na kwa namna hiyo presha inazidi kupanda kwa kocha mkuu wa kikosi hicho Ole Gunnar Solskjaer kutokana na kukosa matokeo ya kuridhisha siku za hivi karibuni.