Kipa Aishi Manula wa Simba sc anatajwa kujiunga na klabu ya Mamelod Sundowns kuchukua nafasi ya Dennis Onyango anayekaribia kustaafu soka baada ya hivi karibuni kustaafu kuchezea timu ya taifa ya Uganda.
Manula ameonyesha kiwango bora hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika hivyo wasauzi hao kuvutiwa nae na kuangalia uwezekano wa kumsajili kipa huyo.
Inasemekena Mamelod imeandaa kiasi cha zaidi ya milioni 500 kumnasa kipa huyo na tayari wameshaulizia upatikanaji wake kwa Simba sc.