Uongozi wa Klabu ya Mbao FC umekubaliana na kocha wao mkuu Hemed Suleiman Morocco kuvunja mkataba wa kuendelea kuifundisha klabu hiyo yenye makao yake makuu mkoani Mwanza.
Inasemekana chanzo cha kuvunja mkataba huo ni mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha ya timu hiyo ambayo
kwa sasa inashika nafasi ya 18 kwenye msimamo ikiwa na alama 19 baada ya michezo 22 ya ligi kuu Tanzania bara.
kwa sasa inashika nafasi ya 18 kwenye msimamo ikiwa na alama 19 baada ya michezo 22 ya ligi kuu Tanzania bara.
Tangu Jana Kocha Morocco alithibitisha kwamba yeye na msaidizi wake Abdulmutik wameondoka jijini mwanza na sasa wako kwao Visiwani Zanzibar huku akisema pande zote mbili zimeachana kwa Amani baada ya kukubaliana kuvunja mkataba.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.