Klabu ya Tottenham imemteua Jose Mourinho kuwa kocha mpya wa klabu hiyo akichukua nafasi ya Mauricio Pochetino ambaye amefukuzwa kutokana na matokeo mabaya kwa siku za hivi karibuni.
Mourinho (56) amesaini mkataba wa miaka mitatu ambao utadumu mpaka mwaka 2023 ili kuleta mataji klabuni hapo baada ya Pochetino kushindwa kuleta taji lolote tangu ateuliwe mwaka 2014 na kufanya timu hiyo kutochukua kombe lolote tangu mwaka 2008.
Pochettino amefukuzwa klabuni hapo baada ya kudumu kwa miaka mitano huku mtendaji mkuu wa klabu hiyo Daniel Levy alisema “kwa Mourinho tumepata meneja mwenye mafanikio duniani”.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.