Site icon Sports Leo

Mtibwa Yamrejesha Carlinhos Kikosini Yanga sc

Taarifa za ndani ya klabu ya Yanga sc zinadai kuwa kocha Cedrick Kaze amemrejesha kikosi cha kwanza kiungo sukari Carlos Carlinhos baada ya kuwa nje kutokana na kutokua fiti baada ya kupata majeraha.

Awali kiungo huyo alikua katika kikosi cha kwanza kilichokua kinaanza michezo tofautitofauti lakini baada ya kukubwa na majeraha nafasi yakeilichukuliwa na Farid Mussa ambaye ametamba kikosini humo kwa muda mrefu.

Kufuatia staa huyo kufunga bao kali lililoshusha presha klabuni hapo sasa amerejeshwa rasmi kikosi cha kwanza cha klabu hiyo huku akijiandaa kuanza katika mchezo dhidi ya Kengold ambapo atacheza winga ya kushoto nafasi ambayo anatumika Farid Mussa.

Exit mobile version