Wakala wa wachezaji Tonombe Mukoko na Tuisila Kisinda, Nestroy Mukwale, amethibitisha kwamba amepokea jumla ya ofa tano zinazowahitaji nyota hao wanaoitumikia klabu ya Yanga.
Akiongea na baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini Mukwale amesema kati ya ofa hizo tatu zinahitaji huduma ya Mukoko na mbili Tuisila. Amesema ni suala la Yanga tu kuamua kufanya biashara au kubaki nao.
Wachezaji hao wamekua na mchango mkubwa kwa Yanga sc msimu huu kiasi cha kuwavutia mawakala mbalimbali duniani huku ikionekana dhahiri klabu hiyo inahitaji kuendelea nao.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.