Kikosi cha klabu ya Simba sc kimewasili salama mjini Kinshasa nchini Congo katika kuelekea mchezo wa klabu bingwa hatua ya makundi dhidi ya As vita Club utakaofanyika siku ya ijumaa.
Kikosi kinacokadiriwa kuwa na wachezaji 27 huku zaidi ya msafara mzima ukijumuisha viongozi na benchi la ufundi ukiwa na takribani zaidi ya watu 40.
Simba sc inabebwa zaidi na uhusiano wake wa karibu na klabu ya Tp mazembe ambao walikua nchini siku za hivi karibuni kucheza michuano ya Simba Super Cup ambao wamekuwa wakiwapa taarifa za ndani zaidi kuhusu As vita.
As Vita wanategeme zaidi video za mchezo wa ligi kuu waliocheza Simba sc dhidi ya Azam Fc kama njia pekee ya kupata kufahamu zaidi kuhusu kikosi cha Simba sc.