Mshambuliaji Taifa Stars na TP Mazembe ya Thomas Ulimwengu amezidi kung’aa Ligi Kuu Congo baada ya kuipatia ushindi timu yake wa 1-0 vs Dauphin Noir.
Goli la Ulimwengu linamfanya afikishe jumla ya magoli 4 ktk Ligi 2020/21 akiwa nafasi ya 2 kwa vinara wa magoli.
Mchezaji huyo hivi karibuni amekua akifanya vizuri tangu ajiunge na miamba hiyo baada kujiunga nao akitokea nchini Algeria Js Saoura huku pia akipitia ligi kuu nchini Sudan.