Mshambuliaji wa Singida BS, Habibu Kyombo ametozwa faini ya Tsh milioni moja kwa kosa la kufanya vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina katika mchezo kati ya Singida Fontaine Gate FC dhidi ya Namungo FC.
Kyombo alionekana akimwaga kimiminika katika goli la klabu ya Namungo katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Majaliwa, Ruangwa na kumalizika kwa ushindi wa 3-2 kwa Singida Fontaine Gate FC.
Bodi ya ligi nchini imetoa adhabu hiyo kwa mshambuliaji huyo kwa kuzingatia kanuni ya 41:5(5.5) ya ligi kuu ambayo inahusu udhibiti wa wachezaji.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Kyombo mshambuliaji wa zamani wa Mbao Fc na Simba sc amekua na kiwango kizuri siku za hivi karibuni akitupia magoli mawili katika mchezo dhidi ya Ihefu Fc uliofanyika katika uwanja wa liti mkoani Singida.