Inasemekana mkataba wa Stephen Sey na klabu ya Namungo unafikia tamati mwishoni mwa msimu huu na klabu ya Yanga iliyopanga kusafisha kikosi chake kwa kuondoa zaidi ya wachezaji tisa wanamuona Sey kama mtu sahihi kuimarisha eneo la ushambuliaji kwenye timu ya wananchi.
Awali klabu hiyo ilifanya usajili mkubwa kwa kuwaleta Yacouba Sogne,Michael Sarpong ambao walitarajiwa kuleta mabadiliko lakini hali haikuwa sawa ndipo akaja Fiston AbdulRazack ambae mpaka sasa bado hajaonyesha kiwango tarajiwa hivyo klabu hiyo inamuona Sey kama mbadala.