Home Soka Yanga Sc,Azam Fc Zakwepana Crdb Cup

Yanga Sc,Azam Fc Zakwepana Crdb Cup

by Sports Leo
0 comments

Klabu za Yanga sc na Azam Fc zitakutana na klabu za Tabora United na Namungo katika hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho la Crdb baada ya droo iliyofanyika leo katika makao makuu ya Azamtv Tabata jijini Dar es salaam.

Azam Fc na Yanga sc hazitakutana mpaka fainali endapo zitafuzu hatua za robo na nusu kutokana na droo hiyo ambapo endapo Yanga sc ataifunga Tabora United basi atakutana na mshindi kati ya Ihefu Fc dhidi ya Mashujaa huku Azam Fc akimfunga Namungo sc basi atakutana na mshindi baina ya Coastal union dhidi ya Geita Gold Sc.

Mechi hizo zinatarajiwa kuchezwa kati ya Mei 2-4 mwaka huu ambapo Yanga sc na Azam Fc zote zitaanzia nyumbani na endapo zitapata sare basi zitarudiana ugenenini ili kupata mshindi wa jumla huku pia akikosekana mshindi katika michezo yote miwili basi hatua ya matuta itaamua mshindi.

banner

Yanga sc ni mshindi wa taji la ngao ya jamii mara mbili mfululizo ambapo akishinda na msimu huu basi atakua amechukua taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited