Home Makala Azam Fc Yaibamiza Prisons Fc

Azam Fc Yaibamiza Prisons Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imefanikiwa kuibuka na alama tatu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons uliofanyika katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaam baada ya kuifunga timu hiyo 3-0.

Mchezo huo uliokua wa kasi uliwashuhudia Azam Fc wakipata bao la kwanza kupitia kwa mchezaji wa Prisons Fc Yona ambaye alijifunga dakika ya 5 huku Abdul Sopu akifunga dakika ya 48 kwa shuti kali na kumshinda golikipa wa Prisons Fc huku Kipre Jr alifunga bao la tatu dakika ya 70.

Kufuatia ushindi huo Azam Fc sasa imefikisha alama 43 katika michezo ishirini ya ligi kuu ikiwa katika nafasi ya pili ya msimamo huku Yanga sc ikiwa katika nafasi ya kwanza na Simba sc ikiwa katika nafasi ya tatu huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited