Home Makala Yanga Princess Yaibuka Mbabe Kwa Simba Queens

Yanga Princess Yaibuka Mbabe Kwa Simba Queens

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya wanawake ya Yanga sc imefanikiwa kuchukua alama tatu muhimu mbele ya Simba queens baada ya kuifunga kwa bao 1-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Wanawake nchini uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex Jijini Dar es Salaam.

 

banner

Yanga Princess imepata ushindi huo muhimu mbele ya Simba queens na kufanya sasa iwe imepata ushindi wa pili katika michezo 13 iliyozikutanisha timu hizo ambapo Simba queens imeshinda michezo tisa na sare mbili.

Bao pekee katika mchezo huo lilipatikana dakika ya 49 likifungwa na Jeannine Mukandayisenga akipiga shuti lililojaa wavuni moja kwa moja ambapo juhudi za kusawazisha hazikuzaa matunda kwa Simba queens.

Yanga Princess kwa miaka ya hivi karibuni wamezidi kuimarika hasaal tangu kocha Edna Lema arejee klabuni hapo ambapo wamefanya sajili za maana zinazosaidia timu kupata matokeo.

Baada ya kupata ushindi huo sasa Yanga Princess wamefikisha alama 30 katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu ya Wanawake nchini huku Simba queens pamoja na kufungwa bado wapo kileleni wakiwa na alama 34.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited