Home Soka Ndayiragije Achomoka Azam

Ndayiragije Achomoka Azam

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha Ettiene Ndayiragije amejiuzulu nafasi yake ya ukocha mkuu wa klabu ya Azam fc huku ripoti zikibainisha anakwenda kujiunga na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa stars) kama kocha mkuu baada ya kukaimu nafasi hiyo kwa muda.

Ettiene raia wa Burundi alikaimu nafasi hiyo baada ya aliyekua kocha mkuu Emmanuel Amunike kutimuliwa kutokana na kufanya vibaya katika michuano ya mataifa ya Afrika (Chan) yaliyofanyika nchini Misri.

Tayari klabu ya Azam imemleta aliyewahi kuwa kocha wa klabu hiyo Aristica Cioaba kuja kuchukua nafasi hiyo iliyoachwa wazi na inatarajiwa mchana wa leo kufanyika hafla rasmi ya kumuaga kocha huyo na kumtambulisha rasmi Cioaba.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited