Kocha Frank Lampard ana kazi kubwa ya kuhakikisha anaibuka na ushindi katika michezo ya ligi kuu nchini humo huku akikabiliwa na majeruhi hasa ya wachezaji muhimu kikosini humo.
Lampard atawakosa beki kisiki Antonio Rudiger huku pia akimkosa Ross Barkley baada ya wote kupata majeraha huku Rudiger akiwa amejitonesha baada ya kuwa ameanza mazoezi akitoka kufanyiwa upasuaji wa mguu.
Ross Barkley akipewa siku kumi za mapumziko kufuatia kuwa majeraha na Kiungo Mason Mount akiwa na hatihati mpaka uchunguzi wa kina kuhusu afya yake ufanyike.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Ruben Loftus Cheek naye yupo kitandani akijiuguza na maumivu ya kiwiko aliyopata wakati akiitumikia klabu hiyo.