Home Soka Lukaku Amtuliza Ibrahimovich

Lukaku Amtuliza Ibrahimovich

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha Inter Milan kimeibuka na ushindi wa magoli 4-2 dhidi ya mahasimu wao, AC Milan katika mchezo wa ligi kuu nchini Italia(Serie A)

Zlatan Ibrahimovic, ambaye amerejea katika ligi kuu ya Italia hivi karibuni, aliifunga timu yake zamani ya Inter (45′) na kutengeneza goli lingine lililofungwa na Ante Rebic (40′), na kufanya hadi halftime, AC Milan, kuongoza kwa magoli 0-2.

Kipindi cha pili Inter waliamka na Marcelo Brozovic na Matias Vecino, waliifungia Milan magoli ya haraka katika dakika ya 51′ na 53′, na kufanya ubao usome 2-2.

Vijana hao wa Antonio Conte walichukua uongozi dakika 20 baadae, baada ya beki, Stefan De Vrij kufunga goli kwa kichwa, kabla ya nyota wa Ubelgiji, Romelu Lukaku, kupigilia msumari wa mwisho katika dakika ya 90.

Inter wamefikisha alama 54 katika msimamo wa ligi ya Serie A, wakiwa alama sawa na vinara wa ligi hiyo kibibi kizee cha Turin,Juventus

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited