Home Makala Ramadhani Hii,Ozil Amekuwa Msaada

Ramadhani Hii,Ozil Amekuwa Msaada

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa Arsenal,Mesut Ozil ameonyesha utu wa kuwajali wengine  baada ya hivi karibuni kutoa kiasi cha pauni 80,000 (sh milioni 231) kwa lengo la kuwasaidia waislamu ambao wameathirika na janga la virusi vya Corona katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani.

Nyota huyo ambaye ni raia wa Ujerumani mwenye asili ya Uturuki atasaidia chakula kwa ajili ya Waislamu 16,000 kwa kipindi chote cha mwezi wa Ramadhan ulioanza April kwa  kusaidia kufuturisha maeneo magumu ya nchini Uturuki.

 

banner

Ozil anapokea mkwanja mrefu ndani ya Arsenal , ambao ni pauni 350,000 pia amekuwa ni mtoaji mzuri kwani amekuwa akiwalisha watu 100,000 wasio na makazi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited