Home Soka Real Madrid Wajichimbia Kileleni

Real Madrid Wajichimbia Kileleni

by Sports Leo
0 comments

Ikiwa imesalia michezo miwili kumalizika kwa ligi ya La liga,Klabu ya Real Madrid inahitaji kushinda mchezo ujao ili kutangazwa mabingwa wa ligi hiyo baada ya jana kufanikiwa kuwafunga Granada mabao 2-1.

Mabao ya Ferland Mendy na Karim Benzema yalitosha kuwahakikishia alama tatu muhimu vijana hao wa Zinedine Zidane hivyo kuhitaji alama tatu tu ili kutangazwa mabingwa wa ligi hiyo.

Real Madrid itawavaa Villareal siku ya Alhamis pamoja na Leganes siku ya jumapili na wakishinda mchezo mmojawapo au kutoa sare michezo yote watakua mabingwa wa ligi hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited