Home Makala Kissu Amwaga Wino Azam Fc

Kissu Amwaga Wino Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

David Mapigano Kissu ametambulishwa rasmi kuwa mali ya Azam Fc baada ya kusaini kandarasi  ya miaka miwili akitokea klabu ya  Gor Mahia ya Kenya.

Kissu alichezea timu za Njombe Mji na Singida United kabla ya kutimkia nchini Kenya pia alikuwa sehemu ya kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kabla ya janga la virusi vya Corona halijasimamisha masuala ya michezo.

Akiwa na Gor Mahia amecheza jumla ya mechi 15 huku akiwa hajaruhusu nyavu zake kuguswa (clean sheet) katika mechi tisa kati ya hizo na timu yake ilitangazwa kuwa mabingwa wa ligi ya Kenya.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited