Home Makala Kocha Na Wachezaji 2 Wakutwa Na Corona

Kocha Na Wachezaji 2 Wakutwa Na Corona

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha Mkuu wa West Ham United, David Moyes pamoja na wachezaji wawili wamekutwa na virusi vya Corona jana kabla ya kuanza raundi ya tatu ya mchezo wao wa Carabao Cup dhidi ya Hull.

Issa Diop na Josh Cullen ndio wachezaji waliokutwa na maambukizi ya Corona huku uongozi wa West Ham United ukithibitisha kwa taarifa hizo kuwa kwa sasa kocha huyo na wachezaji hao wapo chini ya uangalizi wa madaktari hadi afya zao zitakapokuwa salama.

Katika mchezo huo wa jana West Ham ilishinda kwa mabao 5-1 huku kocha msaidizi, Alan Irvine alichukua majukumu ya kukiongoza kikosi hicho kwa kipindi chote ambacho David Moyes atakuwa katika uangalizi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited