Home Makala Man United Yapigwa Chini Kwa Ansu

Man United Yapigwa Chini Kwa Ansu

by Dennis Msotwa
0 comments

Barcelona Imekataa Ofa ya euro 150 milioni iliyowekwa Mezani kwa klabu inayodhaniwa,Manchester United kutoka kwa wakala wa Ansu Fati ili kukamilisha usajili wake.

Manchester United ilitarajia kulipa ofa hiyo kwa awamu mbili ikiwa mwanzo euro 125 milioni na baadaye itaongezwa kutokana na kiwango atakachokionyesha,lakini barca imegoma kabisa kuingia kwenye mazungumzo kwa ajili ya kumuuza nyota huyo.

Ansu mwenye umri wa Miaka 17 amerefusha mkataba wake ambao ulitakiwa kumalizika 2022 na sasa unatarajiwa kufikia kikomo mnamo 2024 huku klabu itakayotaka kumnunua baada ya kumaliza muda huo inabidi kuweka euro 400 milioni mezani ili kumpata kinda huyo.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited