Barcelona Imekataa Ofa ya euro 150 milioni iliyowekwa Mezani kwa klabu inayodhaniwa,Manchester United kutoka kwa wakala wa Ansu Fati ili kukamilisha usajili wake.
Manchester United ilitarajia kulipa ofa hiyo kwa awamu mbili ikiwa mwanzo euro 125 milioni na baadaye itaongezwa kutokana na kiwango atakachokionyesha,lakini barca imegoma kabisa kuingia kwenye mazungumzo kwa ajili ya kumuuza nyota huyo.
Ansu mwenye umri wa Miaka 17 amerefusha mkataba wake ambao ulitakiwa kumalizika 2022 na sasa unatarajiwa kufikia kikomo mnamo 2024 huku klabu itakayotaka kumnunua baada ya kumaliza muda huo inabidi kuweka euro 400 milioni mezani ili kumpata kinda huyo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.