Kutokana na mvua kubwa kunyesha leo Jijini Dar-es-salaam,imepelekea mechi ya kirafiki ya Simba Sc dhidi ya Ndanda Fc kughairishwa.
Mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa leo Octoba 13, majira ya saa 11:00 jioni uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi kwa dhumuni la kuviweka sawa vikosi hivyo katika michuano yao ijayo na timu zingine.
Simba Sc ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu ,kwa sasa inashiriki ligi kuu bara msimu wa 2020/2021 huku Ndanda Fc iliyoshuka msimu uliopita wa 2018/2019 inashiriki ligi daraja la kwanza tayari kujiweka sawa kwa msimu ujao wa ligi.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.