Klabu ya Azam Fc imeonyesha nia ya kumchukua kocha George Lwandamina kuifundisha klabu hiyo baada ya kumtimua kocha Arstica Cioaba kutokana na matokeo yasiyoridhisha.
Taarifa za ndani zinadai kuwa upo uwezekano mkubwa wa kumchukua kocha huyo wa zamani wa Yanga sc na Zesco United ili kujiunga na timu hiyo iliyoanza msimu huku pia ikiangalia uwezekano wa kumchukua Mwinyi Zahera endapo itamkosa mzambia huyo.