Licha ya dili kuvurugika dakika za mwishoni msimu uliopita klabu ya Yanga sc imerudi katika mbio za kumsajili beki Erick Rutanga ambaye ilighairi kumsajili dakika za mwishoni Msimu uliopita.
Inadaiwa kuwa klabu hiyo haijaridhishwa na kiwango cha Adeyum Salehe hivyo inafikiria kuachana nae katika dirisha dogo na imeanza kumtafuta beki huyo anayekipiga Polisi Sc ya nchini Rwanda.
“Nikiwa Rayon Sports nilitakiwa nijunge na Yanga ambao tayari tulikuwa tumeshakubaliana kwa mambo mengi lakini mwisho wa siku mambo hayakunyooka.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
“Katika dirisha hili dogo la usajili naona Yanga wamerudi tena, hivyo siwezi kuzungumza lolote juu ya hili jambo, tutaona litakavyokuwa,” amesema beki huyo.