Licha ya kujitahidi kulinda mabao mawili iliyoyapata dakika za 23 na 69 kupitia kwa Baraka Majogoro na Edward Charles dakika tisini za mchezo dhidi ya Guinnea zilimalizika kwa sare ya 2-2 iliyowalazimu Stars kuaga michuano ya Chan inayoendelea nchini Cameroon.
Guinnea walikua wa kwanza kupata bao dakika ya 4 kwa penati kupitia kwa Yacouba Barry baada ya Carlos Protas kuunawa mpira ndani ya box huku Stars wakirudi na kufunga mabao mawili lakini dakika ya 82 Victor Cantabadouna alisawazisha na kuipeleka Guinnea hatua ya Robo fainali.
Stars na Namibia zinarejea nyumbani huku Zambia na Guinnea wakisonga mbele katika kundi hilo D.