Home Soka Kim Awabeba Matola,Mgunda

Kim Awabeba Matola,Mgunda

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Taifa Stars Kim Poulsen amelibakisha benchi lote la ufundi lilokuwa likitumiwa na Ettienne Ndayilagije wakiwemo makocha wasaidizi Selamani Matola na Juma Mgunda.
“Benchi la ufundi litabaki lilelile kama lilivyokuwa, nilikuwa na mazungumzo mazuri na Mgunda pamoja na Matola lakini pia nimeshakutana na Matola na tumeongea”.Alisema Kim
“Pamoja na kocha wa makipa na kocha wa viungo watabaki vilevile sikuona sababu ya mimi kuja hapa na kubadilisha kila kitu, ingawa akija kocha mpya anaangalia ni kivipi unafanya kazi yako, kikubwa kila mtu atimize majukumu yake vizuri kuanzia kwa wachezaji hadi benchi la ufundi,”
Kwa sasa Matola ni kocha msaidizi wa klabu ya Simba, huku Mgunda akiwa kocha mkuu wa klabu ya Coastal Union.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited