15
Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limetoa mwongozo kwa klabu zitakazoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho msimu ujao wa 2021/2022 ni lazima kocha mkuu awe na leseni A na kocha msaidizi lazima awe na leseni B.
Kwa kocha yeyote ambaye atakuwa hajakidhi vigezo hivyo hataruhusiwa kukaa kwenye benchi la ufundi katika timu yeyote iliyopo katika michuano hiyo.
Hii inamaanisha kuwa vigezo hivi vitambana kocha msaidizi wa Simba Seleman Matola ambaye ana leseni C endapo atakuwa hajajiendeleza na kupata leseni B