Home Soka Ugonjwa Wambakisha Ajibu Dar

Ugonjwa Wambakisha Ajibu Dar

by Sports Leo
0 comments

Wakati msafara wa kikosi cha Simba sc ukielekea jijini Mwanza kuwavaa Polisi Tanzania,mchezaji Ibrahim Ajib hajasafiri na kikosi hicho kutokana na kusumbuliwa na maumivu hali iliyomfanya kutohudhuria mazoezi ya timu.

Kwa mujibu wa kocha wa kikosi hicho Didier Gomez mchezaji huyo hakuhudhuria mazoezi ya siku mbili katika uwanja wa Mo Simba Arena hali iliyomfanya amuache katika kikosi hicho huku akitarajia kuungana nae jumapili katika maandalizi ya michezo mingine.

“Ajibu kama atakuwa na maendeleo mazuri ya kiafya tunategemea kuwa nae katika kikosi Jumapili na ataungana na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya mechi nyingine zinazofuata,” alisema Gomes.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited