Home Makala Injinia Amkataa Ajibu

Injinia Amkataa Ajibu

by Sports Leo
0 comments

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano Injinia Hersi Said amesema kiungo wa Simba Ibrahim Ajibu sio miongoni mwa wachezaji watakaovaa uzi wa Yanga msimu ujao.

Siku za karibuni kuliibuka tetesi zilizomuhusisha Ajibu kusajiliwa na Yanga. Ni tetesi zilizoibua makundi miongoni mwa mashabiki wa Yanga wengine wakipinga usajili huo huku wengine wakiunga mkono.

Injinia Hersi amesema Ajibu sio miongoni mwa wachezaji walio katika mpango wa usajili wa mabingwa hao wa kihistoria.

banner

Aidha amedokeza kuwa tayari wamekamilisha usajili wa baadhi ya wachezaji ambao watatambulishwa wakati mwafaka ukifika

Hakuna shaka miongoni mwa wachezaji hao ni mlinzi wa kulia Djuma Shaban anayetua kutoka klabu ya AS Vita huku akisema kutakuwa na utaratibu tofauti wa kutambulisha wachezaji wapya

“Ndio tutakuwa na utaratibu wa utambulisho wa wachezaji wapya, tutawaeleza kupitia vyombo vyetu rasmi, sio yeye tu (Djuma) ila na wengine ambao tutakuwa tumemalizana nao,” Injinia Hersi aliiambia Clouds Fm

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited