Home Soka Yanga sc Wakatisha Kambi Morroco

Yanga sc Wakatisha Kambi Morroco

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imekatisha ratiba ya kambi ya maandalizi kujiandaa na michuano mbalimbali inayoendelea nchini Morroco kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuitwa kwa baadhi ya mastaa kujiunga na timu zao za Taifa.

Mpango huo wa kusitisha kambi umetangazwa na kaimu mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo Eng.Hersi Said ambapo sassa italazimika mastaa wa timu hiyo kurejea nchini haraka kuendelea na mazoezi kwa siku kadhaa zilizosalia kabla ya kufika kilele cha siu ya mwananchi kinachofanyika siku ya jumapili Septemba 29 jijini Dar es salaam.

Yanga sc ina kazi kubwa ya kutafuta muunganiko wa timu kufuatia kusajili mastaa wapya kikosini wakiwemo mastaa wa kimataifa ambao pia wanahitaji kuzoea mazingira ya hali ya hewa nchinin ili kuleta ufanisi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited