Home Soka Koffi Atua Dar Kuipamba Siku ya Wananchi

Koffi Atua Dar Kuipamba Siku ya Wananchi

by Sports Leo
0 comments

Nguli wa mziki wa Bendi barani Afrika Koffi Olomide ametua nchini ambapo atasherehesha tukio la siku ya wananchi liliandaliwa na klabu ya Yanga sc ikiwa ni siku maalumu ya kufanya utambulisho wa wachezaji wapya kwa ajili ya msimu wa ligi kuu nchini 2021/2022.

Koffi akiwa sambamba na wasaidizi wake ametua leo uwanjani na kupokelewa na afisa habari mpya wa klabu ya Yanga sc Haji Manara aliyekua na kundi la mashabiki kadhaa waliojitokeza kumpokea mwanamuziki huyo mkubwa mwenye vibao vikali.

Mpaka sasa tiketi za tamasha hilo zimenunuliwa kwa wingi na mashabiki wa klabu hiyo huku tayari tiketi za watu mashuhuri zikiwa zimeisha zikibaki za watu mashuhuri daraja la tatu na mzunguko ambazo zinauzwa elfu 20 na elfu 5.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited