Home Makala Guardiola aambiwa abaki kuwa kocha tu

Guardiola aambiwa abaki kuwa kocha tu

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola ameambiwa na mashabiki wa klabu hiyo kuwa anatakiwa abakie kufanya majukumu yake ya kuifunza timu badala ya kuingilia na kuwaambia mashabiki nini cha kufanya.

Pep alilamika uchache wa mashabiki wa timu hiyo walijojitokeza kushuhudia mchezo wa michuano ya klabu bingwa Ulaya kwenye mkutano na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mchezo huo dhidi ya RB Leipzig walioshinda 6-3.

Mkufunzi huyo alisema kuwa mashabiki wanapaswa kujitokeza kwa wingi katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Southampton kwani wamefunga mabao 16 katika michezo mitatu hapo Etihad hivyo mashabiki wanapaswa kuhamasika,akionesha kutoridhishwa na mahudhurio.

banner

Katika wa klabu ya mashabiki wa Man City alisema ”Pep ni kocha bora duniani nadhani anatakiwa kubakikuwa hivyo,haelewi ugumu ambao mashabiki wanaweza kuwa wanapitia katika dimba la Etihad hasa mechi za katikati ya juma.Wana watoto kuwahudumia wakati mwingine hawawezi kumudu gharama za tiketi.Lakini pia kuna maswala ya Uviko-19 hivyo sielewi kwanini analalamika”.

Guardiola amekuwa akilalamika kukosekana kwa hamasa ya mashabiki wa Man City kuhudhuria na kuipa nguvu timu hiyo hwaswa kwenye michuano ya klabu bingwa Ulaya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited