Home Soka Ansu Fati asaini mkataba mpya Barca

Ansu Fati asaini mkataba mpya Barca

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji kinda wa FC Barcelona Ansu Fati amesaini mkataba wa miaka sita kuendelea kukipiga katika viunga vya Nou Camp hadi mwaka 2027 huku kukiwa na kipengele cha kumsajili chenye thamani ya Euro bilioni moja.

Huo ni muendelezo wa klabu hiyo kuendelea kuwatia vitanzi wachezaji wao makinda baada ya awali kumsainisha Pedri mkataba mpya,hali hiyo ni kama tahadhari ya kuhofia kuwapoteza hasa kipindi hiki timu hiyo ikipitia ukata mkubwa katika historia ya klabu hiyo.

Taarifa rasmi ya klabu ya twitter imethibitisha hilo

banner

Barca wapo kwenye mazungumzo na wachezaji wengine makinda Pablo Gavira,Oscar Mingueza na Ronald Araujo kuwaongezea mikatabu mipya.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited