Home Soka Usain Bolt alia Conte kutua Spurs

Usain Bolt alia Conte kutua Spurs

by Dennis Msotwa
0 comments

Mwanariadha maarufu duniani kutoka Jamaica amesema kuwa anasikitishwa sana na kocha Antonio Conte kujiunga na Tottenham Hotspurs ya Uingereza kwani alitamani sana kocha huyo kutua Man United.

Bolt ni shabiki mkubwa sana wa mashetani wekundu Man Utd na mara kwa mara amekuwa akihudhuria michezo ya nyumbani ya timu hiyo na mara kwa mara amekuwa akionesha hisia zake kwa klabu hiyo kupitia mitandao yake ya kijamii.

Akihojia na skysports Bolt amesema kuwa Conte ni kocha mshindi na mwenye uwezo mkubwa sana wa kufundisha soka,amethibitisha hilo kila alipokwenda kwa kutwaa mataji na kama angetua Old Trafford basi angeirejesha klabu yake kwenye zama za mataji.

banner

Aliendelea kusema kuwa hongera kwa Spurs kumpata kocha huyo kwani ataiunganisha timu hiyo na kuifanya kuwa moja ya timu tishio barani Ulaya endapo watamtimizia mahitaji yake.

Kauli ya mwanariadha huyo anayeshikiria rekodi mbalimbali za dunia kwenye riadha inaonesha kuwa hana imani tena na kocha Ole Gunnar Solskjaer ambaye yupo kwenye shinikizo la kufukuzwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited