Home Kikapu Chicago Bulls Yamkabidhi Billy Donovan Mkataba wa Mpya

Chicago Bulls Yamkabidhi Billy Donovan Mkataba wa Mpya

by Dennis Msotwa
0 comments

Chicago Bulls imetangaza kuwa wamekabidhi mkataba wa nyongeza ya muda mrefu kwa kocha wao wa mkuu Billy Donovan kutokana na kazi njema aliyoifanya klabuni hapo kwa msimu ulioisha.

“Billy ni mwenye ujuzi na uwezo mkubwa wa kuongoza,” alisema Makamu wa Rais wa Bulls, Arturas Karnisovas. “Tunaamini kuwa ana uwezo wa kuleta mafanikio kwa timu yetu kwa miaka ijayo.”Alimalizia kusema bosi huyo mwenye ushawishi klabuni hapo.

Donovan alijiunga na Bulls mwaka 2020, na kwa sasa ameongoza timu kwa msimu wa pili mfululizo wa playoffs ambapo alinukuriwa akisema yafuatayo baada ya kusaini mkataba huo mpya ambao haujafahamika ni wa muda gani.

“Ninashukuru familia ya Bulls kwa imani yao,” alisema Donovan. “Nina hamu ya kuendelea kufanya kazi na wachezaji wetu wa kipekee na wataalamu wa klabu hii.”Alisema kwa hisia kali.

Bulls wameanza msimu wa 2023-24 kwa rekodi nzuri, na wanaamini kuwa Donovan ataendelea kuwaongoza kwenye mashindano ya juu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited