Home Kikapu Mannon Asaini Miwili Lakers

Mannon Asaini Miwili Lakers

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Los Angels Lakers imemsaini mchezaji mpya wa nafasi ya ulinzi Chris Mañon kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kuonesha uwezo wake kwenye ligi za majira ya joto za Golden State Warriors yanayoendelea nchini marekani.

Lakers walikubaliana na Mañon Alhamisi hii kuhusu dili hilo la staa huyo ambaye alicheza msimu uliopita kwenye chuo cha Vanderbilt baada ya kutumia miaka mitatu kwenye chuo cha Cornell ambapo katika misimu yake yote minne ya chuo, aliwahi kufunga wastani wa vibao 1.7 kwa kila mchezo.

Baada ya kutochaguliwa kwenye drafti hilo Mañon aliichezea Warriors kwenye mashindano ya California Classic huko Las Vegas mwezi huu, akivutia macho kwa uchezaji wake mzuri kwenye mashambulio na ulinzi.

Mañon alifunga pointi 8, kupata rebound 3,na kufanikiwa kukamata mpira mara 3, na kuzuia mipira mara mbili 2 wakati Warriors walipoishinda Lakers kwenye mchezo wa kwanza wa California Classic.

Kwa ujumla msimu uliopita,alimaliza ligi za majira ya joto kwa wastani wa pointi 9.0, rebound 4.3, asisti 1.9, kukamata mpira 1.6, na kuzuia risasi 1.4 katika michezo saba.

Lakers walimrudishia mkataba wa miaka miwili mchezaji mrefu Christian Koloko mapema wiki hii. Mkataba wa Mañon unawaacha na nafasi moja tu ya mkataba wa miaka miwili kwa sasa kati ya mastaa wanaokaribia kumaliza mikataba klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited