Timu ya Golden State Warriors, imeendelea kufanya vibaya msimu huu baada ya kukubali kichapo cha pointi 108-114 dhidi ya timu ya Oklahoma Thunder.
Licha ya nyota mpya wa Warriors, D’Angelo Russell, kufunga pointi 30 lakini hazikutosha kuiepusha na kipigo kutoka kwa Oklahoma.
Warriors wameonekana kufanya vibaya msimu huu, baada ya kuwakosa nyota wao watatu, Stephen Curry, Draymond Green na Klay Thompson, ambao wote ni majeruhi huku Curry akikosa mechi zote zilizosalia za msimuu huu huku siku ya alhamisi watakua ugenini kuvaana na L.A lakers.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.