76
Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo imeanza kutekeleza maelekezo ya Rais John Magufuli wa kubadili jina la Uwanja wa Taifa na kuwa Mkapa Stadium katika kumuenzi rais mstaafu wa awamu ya tatu, hayati Benjamin Wiliam Mkapa.
Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara hiyo, Yusufu Singo ameeleza kuwa mchakato umeshaanza na wameshaliondoa jina la zamani ili kuweka jina la Mkapa, kwa maelekezo ya Waziri wa Michezo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo.
Rais Magufuli alitoa maelekezo ya kubadili jina la uwanja wa Taifa uitwe Uwanja wa Mkapa (Mkapa Stadium)wakati akitoa salamu za rambirambi kwenye kuuaga mwili wa Mkapa, Jumanne hii kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.