Home Makala Aguero Kusepa Man City

Aguero Kusepa Man City

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji  wa Manchester City, Sergio Aguero anaweza kusepa ndani ya kikosi hicho pale mkataba wake utakapofika tamati mwaka 2021 na inaelezwa kuwa ana mpango wa kurejea kwenye klabu yake iliyomkuza ya Independiente ya Argentina.

Nyota huyo raia wa Argentina mwenye miaka 31 alijiunga na Manchester City akitokea klabu ya Atletico Madrid alikodumu kuanzia msimu wa 2006-2011.

Aguero ametupia jumla ya mabao 254 na ndiye namba moja kwa kufunga mabao mengi ndani ya Manchester City ambao ni mabingwa watetezi wa kombe la Ligi Kuu England.

banner

Manchester City inashika nafasi ya 2 katika msimamo wa ligi kuu England ikiwa na pointi 57 katika michezo 28,imeshinda mechi 18 na kutoa sare 3 .

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited