Home Makala Aliyekuwa Rais Wa Madrid Afariki

Aliyekuwa Rais Wa Madrid Afariki

by Sports Leo
0 comments

Rais wa zamani wa timu ya Real Madrid ya Hispania, Lorenzo Sanz amefariki dunia kwa virusi vya corona akiwa na umri wa miaka 76.

Sanz amekuwa akiitumikia timu ya Real Madrid kwa kipindi cha miaka mitano (1995 – 2000) na alipoteza maisha jana wakati akipatiwa matibabu ya virusi vya Corona.

Akiwa madarakani 1998 alifanikisha timu yake ya Madrid kucheza fainali ya kwanza ya michuano ya Ulaya na hata kushinda kombe la ligi ya mabingwa ulaya mara mbili.

banner

Kupitia ukurasa wa twitter mwanaye alisema”Baba yangu amefariki huu ndio mwisho wake kwa sasa, amekuwa kiongozi mzuri na mtu ambaye nimekuwa nikimfuata katika mengi, alikuwa ni mchapakakazi na ni miongoni mwa watu ambao sijawahi kuwaona”.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited