Home Makala Ansu Fati apewa namba ya Messi Barca

Ansu Fati apewa namba ya Messi Barca

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji kinda wa Fc Barcelona Ansu Fati ni kama amekabidhiwa mikoba ya gwiji wa timu hiyo Lionel Messi baada ya uongozi wa klabu hiyo kumkabidhi jezi namba 10.

Jezi namba 10 ilikuwa ikivaliwa na Messi aliyetimkia PSG majira haya ya joto baada ya mkataba wake kumalizika ndani ya Nou Camp na kushindwa kuingia mkataba mpya kutokana na sheria ngumu za la liga juu ya muundo wa mishahara.Messi alipewa jezi hiyo mwaka 2007 kutoka kwa Ronaldinho Gaucho.

Ansu mwenye miaka 18 ni zao la soka kutoka akademi ya Fc Barcelona ijulikanayo kama La Masia na alipandishwa kuitumikia timu ya wakubwa mwaka 2019 ambako alifanya vizuri na kuonesha kuwa atakuja kuwa mchezaji wa kutumainiwa ndani ya klabu hiyo yenye maskani yake katika kitongoji cha Catalan.

banner

Msimu wa 2020/2021 haukuwa mzuri kwa Fati baada ya kuumia na kukaa nje ya uwanja takribani msimu mzima na ndio kwanza amerejea kutoka majeruhi msimu huu.

Ansu Fati licha ya umri wake mdogo ameshaitumikia timu ya taifa ya Hispania na kupewa kwake jezi namba 10 ndani ya Barcelona ni imani kubwa ya Wakatalunya kuwa ataibeba timu hiyo kama alivyofanya mtangulizi wake japo ana viatu vikubwa sana vya kuvaa tokana na ubora mkubwa aliokuwa nao Lionel Messi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited